Vifaa:
- Unga wa ngano
- Mafuta ya kula au Samli
- Hiliki
- Zabibu kavu
- Nazi
- Maji
- Chumvi
- Sukari
- Hamira ya chenga.
- Vanilla flavor
Matayarisho:
- Weka unga wa ngano kwenye chombo cha kukandia, tia hamira ya chenga, chumvi kidogo, hiliki, vanilla, zabibu kavu, sukari na samli au mafuta ya kula kisha anza kuchanganya.
- Ukishachanganya anza kuweka tui la nazi kidogo kidogo huku unakanda, kama unaona unga ni mgumu tia maji huku ukiendelea kukanda.
- Unga ukishakua laini (usiwe laini sana wala mgumu sana) anza kukata madonge kama ya chapati.
- Ukishamaliza sukuma donge moja kwenye kibao cha chapati kisha katakata kwa size na style upendayo.
- Ukishamaliza acha maandazi yaumuke. (Yaache kwa nusu saa).
- Weka kikaango jikoni, mimina mafuta ya kula, weka moto wa wastani kisha anza kuchoma maandazi.
- Yakianza kubadilika rangi kwenda ya brown geuza upande wa pili. Yakiiva toa jikoni, chuja mafuta kwa ajili ya kula.